Showing posts with label BONGO ARTIST. Show all posts
Showing posts with label BONGO ARTIST. Show all posts

April 6, 2015

MAYWEATHER JR VS MANNY PACQUIAO ON MAY 2ND 2015

Hi | 9:12:00 PM | | | Be first to comment
While the weekend was filled with the news about what was going to happen or was happening at the Oscars, boxing fans around the world were still digesting the news about the upcoming fight between Floyd Mayweather and Manny Pacquiao. I am one of them. Unlike many fans who jumped and shouted the word Yes at the top or couldn’t stop singing,humming and chanting, I sat down with the heightened senses calmly saying, “Finally, it is happening”. But I also phoned and texted couple of my close friends to share news or pass on the excitement.

It’s is, without a doubt, one of the most anticipated fights in recent history. A number of things makes this fight special [and I guess that is exactly what Mayweather wanted all along].

Manny and Pacquiao are both very well respected boxers [if that respect is not an understatement] with millions of fans behind their backs. Mayweather has never lost a professional fight. His current record is 47-0. That alone should widen your eyes and make you take a step back. But it’s true. No one has managed to beat him. Whether there is anything behind what we see in the ring or not, only him and his closest buddies know. With his chin high and shoulders back and a gleam in one of his eye, Mayweather is already boasting that come May 3rd his record will be 48-0!

May 22, 2014

MWONGOZAJI “ DIRECTOR” HASA NI NANI KATIKA TASNIA YA FILAMU/SINEMA?

Hi | 1:04:00 AM | | | Be first to comment

Hakuna jibu la moja kwa moja ambalo linaelezea mtu anawezaje kuwa mwongozaji wa filamu.

Swali la msingi la kujiuliza ni kwamba:

Mwongozaji “ Director” hasa ni nani katika tasnia ya filamu/sinema?

jibu lake laweza kuwa ni fupi, ni mtu anayetengeneza taswira ya namna ya kuwasilisha muswada (script) kuwa maisha halisi, anachagua na anawaongoza wahusika kuweza kuwasilisha ujumbe kama ulivyokusudiwa,

Watu wengi wamekuwa wakitamani au kuwa na Ndoto za kuwa waongozaji wenye mafanikio na maarufu kama James Cameroon, Michael Moore, Mery Gibson, Tsai Ming – Ling, Ang Lee, George Lucas, Tim Burton na wengine wengi.

Lakini mafanikio hayo mtu anaweza kuyapata kwa namna gani?.

Mtu anawezaje kuwa mwongozaji wa filamu?

Hakuna jibu lolote la kujitosheleza ambalo lipo na linaelezea ni kwa namna gani mtu anaweza kuwa mwongozaji wa filamu. Ingawa unaweza Kusema kuwa mtu anaweza kuwa mwongozaji wa filamu kwa kuchukua video kamera na kuanza kuongoza.

Swali la msingi hapa ni kwa jinsi gani mtu anaweza kuwa mwongozaji mweledi?

WAONGOZAJI WAZURI WA MOVIE NI WALE WENYE HISTORIA YA UANDISHI WA MUSWADA (SCRIPT)

Hi | 1:00:00 AM | | | Be first to comment
Kazi kubwa ya mwongozaji ni kuhakikisha anatengeneza filamu nzuri na yenye ubora wa kimataifa, akitumia vema vipaji vya waigizaji anaofanya nao kazi. Waongozaji wengi hasa wale wa Hollywood, bollywood walianza safari yao ya kuwa waongozaji kwa kuanza kuigiza, lengo lao likiwa ni kuijua vizuri tasnia ya uigizaji.

Ujuzi wa kuigiza unaweza kuwasaidia wale wote wanaopenda kuwa waongozaji wa filamu kujifunza mbinu na mitindo mbalimbali inayotumiwa na waongozaji mbali mbali kuongoza filamu, ni dhahiri kuwa kila mwongozaji wa filamu ana staili na mtindo wake wa kuongoza filamu.

MAKAMPUNI YANAYOTENGENEZA FILAMU PAMOJA NA TAALUMA

Hi | 12:55:00 AM | | | | | Be first to comment
Taaluma si kitu ambacho watu wengi wanakitilia mkazo hapa kwetu Tanzania hasa kwenye tasnia ya filamu, ukweli utabakia kuwa kipaji pekee hakitoshi kumfanya mtu aweze kuwa mwongozaji bora, taaluma ni kitu cha msingi sana kukipata, waongozaji wote wa filamu duniani wamesomea taaluma ya uongozaji na ndio maana si ajabu kuona kila siku tunaona vitu tofauti na ubunifu wa hali ya juu katika filamu wanazoziongoza.
Waongozaji wengi hasa waliofanikiwa ni wale waliopata elimu ya stashahada au shahada kutoka katika vyuo , shule binafsi na vyuo vikuu zinatoa kozi za sanaa katika mambo ya utangazaji, redio, filamu na televisheni. Ingawa vyuo vingi tulivyonavyo vinatoa zaidi mafunzo ya nadharia katika tasnia ya sanaa, na vyuo vichache vinavyotoa mafunzo ya uongozaji wa filamu/sinema.

Home of Technologies © Copyright 2010-2015 : Designed by : WebMaster