JIUNGE NASI KUPITIA HAPA
TAFUTA CHOCHOTE BLOG
SOMA HABARI KWA MIEZI
SOMA ALAMA ZA NYAKATI
Showing posts with label MICHEZO. Show all posts
Showing posts with label MICHEZO. Show all posts
December 17, 2013
September 18, 2013
FRANCIS CHEKA NAHITAJI KUWA MPYA KIELIMU ILI NIFIKE MBALI NAAMUA KUANZA KIDATO CHA KWANZA
Bingwa wa dunia wa WBF Francis Cheka ambaye hivi karibuni alipewa zawadi ya kiwanja na Rais Jakaya Kikwete baada ya ushindi wake dhidi ya bondia wa Marekani, ameamua kurudi shule.Cheka anasema hakupata nafasi ya kwenda shule kutokana na matatizo ya kifamilia na kuishia darasa la saba. “Mimi sikusoma niliishia darasa la saba, lakini nimeamua kurejea darasani baada ya kupewa udhamini na shule ya St Joseph”.
August 8, 2013
JUMA KASEJA NI NI MIONGONI MWA WADAU WATAKAOHUDHURIA FAINALI YA KOMBE LA MEYA JIJI LA MWANZA - MEYOR'S PEPSI CUP
Na Mashaka Baltazar, MwanzaBALOZI wa Pepsi, Juma Kaseja ni miongoni mwa wa wadau wa soka walioalikwa kushuhudia fainali ya kuwania kombe la Meya wa Jiji la Mwanza (Meyor’s Pepsi Cup ), Stanslaus Mabula.
Mlinda mlango huyo namba moja wa timu ya taifa (Taifa Stars) ataungana na Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makala Katibu Mkuu wa TFF na Angetile Osiah.
Wengine ni Memeya wa Majiji na Miji ya Dar es Salaam Jerry Slaa,
Gaudensi Lyimo wa Arusha, Kapinga wa Mbeya, Omari Nondo wa Morogoro,
Moshi na Bukoba.
Fainali hiyo itafanyika Agosti 10 mwaka huu ambapo bingwa
atajinyakulia pikipiki ya magurudumu matatu (Bajaj) na shilingi milioni
moja, kombe kubwa na dogo na medali za dhahabu wa pili ataibuka na
kitita cha shilingi 1.5 milioni, kombe na medali ya fedha.
June 28, 2013
GOLIKIPA DIDA WA ZAMANI WA SIMBA AJIUNGA NA YANGA MKATABA WA MIAKA 2
Aliyekuwa
golikipa wa timu ya Simba, Azam na Mtibwa Deogratius Munishi maarufu
kama Dida amejiunga rasmi na klabu bingwa ya Tanzania bara - Dar Young
African.
June 16, 2013
SUPPORT OUR NATIONAL TEAM TAIFA STARS
Hi | 3:47:00 PM |
BIASHARA
|
BURUDANI
|
EAST AFRICA
|
JAMII
|
MICHEZO
|
MUSIC
|
SERIKALI
|
UGHAIBUNI
Be first to comment
May 16, 2013
MARTIN SAANYA REFA ATAKAYECHEZESHA PAMBANO LA SIMBA NA YANGA SC LA KUFUNGA PAZIA LA LIGI KUU YA VODACOM
REFA
Martin Saanya kutoka Morogoro ndiye atakayechezesha pambano la watani
wa jadi, Simba na Yanga SC la kufunga pazia la Ligi Kuu ya Vodacom
Tanzania Bara Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Katika
mchezo huo, unaosubiriwa kwa hamu na wapenzi wa soka nchini ili
kujionea nani zaidi baina ya miamba hiyo, Saanya atasaidiwa na Samuel
Mpenzu wa Arusha na Jesse Erasmo kutoka Morogoro, wakati refa akiba
atakuwa ni Hashim Abdallah wa Dar es Salaam.
Kamisaa
wa mechi hiyo atakuwa Emmanuel Kavenga kutoka Mbeya wakati mtathmini wa
waamuzi atakuwa ni Leslie Liunda wa Dar es Salaam.
April 15, 2013
March 20, 2013
February 12, 2013
January 18, 2013
RATIBA YA KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA - 2013
Ratiba nzima ya mashindano ya kombe la mataifa ya Africa yatakayofanyika
kule Afrika ya kusini kuanzia jumamosi ya wiki hii yani tarehe 19, 2013
ambapo mechi ya kwanza itakuwa ni Afrika ya kusini na Cape Verde.
January 17, 2013
December 10, 2012
TASWIRA ZA AFTER SCHOOL BASH 2012
Hi | 11:20:00 PM |
BONGO MOVIE
|
BURUDANI
|
EAST AFRICA
|
EVENTS
|
FASHION
|
MICHEZO
|
MUSIC
Be first to comment
Labels:
BONGO MOVIE,
BURUDANI,
EAST AFRICA,
EVENTS,
FASHION,
MICHEZO,
MUSIC
October 22, 2012
Wateja wa Barclays kushuhudia Ligi Kuu ya England (BPL) live
Mkuu wa Mawasiliano wa Benki ya Barclays
Tanzania, Tunu Towo Kavishe (kushoto) akionyesha jezi halisi ya timu ya
Arsenal ikiwa ni moja ya zawadi watakazopewa washindi wa promosheni ya
Ligi Kuu ya England (BPL) inayoendeshwa na benki hiyo. Mshindi mmoja
katika kila droo hujishindia tiketi ya yeye na mwenzake kwenda
kushuhudia moja ya mechi ya ligi hiyo nchini Uingereza. Droo hiyo
ilifanyika jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Mkaguzi wa Bodi ya
Michezo ya Kubahatisha Tanzania (GBT), Maggid Bakari na Mkuu wa Bidhaa,
Huduma na Utafiti wa benki hiyo, Samwel Mkuyu.
Mkazi wa Jiji la Dar es Salaam, Rukia
Kizwi (kushoto) akitoa tiketi ili kumpata mmoja wa washindi wa
promosheni ya Ligi Kuu ya England (BPL) inayoendeshwa na benki hiyo.
Mshindi mmoja katika kila droo hujishindia tiketi ya yeye na mwenzake
kwenda kushuhudia moja ya mechi ya ligi hiyo nchini Uingereza na wengine
wawili hujishindia zawadi ndogondogo. Droo hiyo ilifanyika jijini Dar
es Salaam jana. Wa pili kutoka kushoto ni Mkuu wa Mawasiliano wa
Barclays, Tunu Towo Kavishe, Mkuu wa Bidhaa, Huduma na Utafiti wa benki
hiyo, Samwel Mkuyu, Mkaguzi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Bakari
Maggid na Ofisa Mawasiliano wa Barlclays, Lilian Machare.
October 18, 2012
NCHI TISA KUSHIRIKI ROCK CITY MARATHON 2012 OKTOBA 28
Mwenyekiti
wa Baraza la Michezo Tanzania, Dioniz Malinzi (wa tatu kushoto) akiwa
katika picha ya pamoja na baadhi ya wawakilishi wa wadhamini wa mbio za
Rock City Marathon 2012, wakifuatilia uzinduzi wa maandalizi ya mbio
hizo
uliofanyika kwenye Hoteli ya New Afrika. Rock City Marathon zitafanyika
Oktoba 28 kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza Oktoba 28.
Ofisa Uhusiano wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Jane Matinde
(kulia) akimkabidhi hundi ya shilingi milioni 5, Meneja Matukio wa Kampuni ya
Capital Plus International ambaye pia ni Mratibu Rock City Marathon
2012, Grace Sanga jijini Dar es Salaam hivi karibuni kama sehemu udhamini wa
mbio hizo zitakazofanyika kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza Oktoba 28
Oktoba. Airtel pia walikabidhi fulana 400 zitakazotumika katika mbio hizo.
Mkali wa Bongo Flava Juma Kassim 'Sir Nature' (katikati) akiimba na
Baby adaha kutambulisha shoo yao kali itakayofanyika sambamba na mbio
za Rock City Marathon 2012. Kushoto ni Mratibu wa mashindano hayo, Grace
Sanga, wa Kampuni ya Capital Plus inayoandaa mashindano hayo.
DAR ES SALAAM, Tanzania
JUMLA ya nchi tisa zinatarajiwa kushiriki katika mbio za
kilomita 21 za Rock City Marathon 2012, zilizoandaliwa na Kampuni ya Capital
Plus International (CPI), zitakazofanyika Jumamosi Oktoba 28 kwenye Uwanja wa
CCM Kirumba jijini Mwanza.
Akizungumza na Tanzania Daima jijini Dar
es Salaam leo, Mratibu wa mbio hizo Grace Sanga wa CPI, alizitaja
nchi hizo kuwa Kenya, Uganda, Rwanda,
Burundi, Jamhuri ya
Kidemokrasia Congo (DRC), Australia,
India, Canada na
Marekani, huku akidokeza maandalizi mazuri yamechangia ongezeo la washiriki.
“Tumetuma mialiko ya kushiriki kwa wadau wote wa riadha wa
nchi jirani ili wapate kushiriki Rock City Marathon 2012, ndio maana tunategemea
kupata washiriki wengi zaidi kutoka nje ya nchi, kulinganisha na mwaka uliopita
na maboresho ya mbio hizi yatachangia kuongeza ushindani,” alisema Grace.
Sanga aliongeza kuwa, mbio hizo za kila mwaka zimegawanywa
katika makundi matano ya mbio za kilomita 21 kwa wanawake na wanaume, kilomita
tano kwa watu wote, kilomita tatu kwa walemavu, kilomita tatu kwa wazee kuanzia
miaka 55 na kilomita mbili kwa watoto wa kati ya miaka saba hadi kumi.
Rock City Marathon zilianzishwa mwaka 2009, ambapo mwaka huu
ziko chini ya udhamini wa NSSF, Airtel Tanzania, Geita Gold Mine, Shirika la
Ndege Tanzania (ATCL), PPF, African Barrick Gold, New Africa Hotel, Nyanza
Bottles, New Mwanza Hotel, TANAPA na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB).
Mbio hizo zinazosubiriwa kwa hamu na wakazi wa Kanda ya
Ziwa, zitapambwa na burudani ya aina yake kutoka kwa nyota wa muziki wa kizazi
kipya nchini Juma Kassim ‘Sir Nature’, ambapo zitaanzia kwenye Uwanja wa CCM
Kirumba kupitia njia tofauti na kurudi uwanjani hapo.
September 2, 2012
SERENA APAA, VENUS WILLIAMS AKIAGA US OPEN 2012
NEW YORK, Marekani
Wakati Serena akisonga mbele, ndugu yake na bingwa wa zamani wa US Open, Venus Williams alijikuta akitolewa mashindanoni kwa kukubali kichapo cha 6-2 5-7 7-5 kutoka kwa Angelique Kerber
NYOTA anayeshika nafasi ya nne katika viwango vya ubora wa tenisi duniani, Serena Williams hakupata shida kufuzu raundi ya tatu ya micuano ya Wazi ya Marekani ‘US Open’ baada ya kupata ushindi wa moja kwa moja dhidi ya Mhispania Maria Jose Martinez Sanchez.
Bingwa huyo wa michuano ya Wimbledon na Olimpiki, alitumia muda wa saa moja na dakika 22 (1:22) kuibuka kidedea kwa seti mbili kwa bila za 6-2 6-4 dhidi ya nyota asiyekuwa na kiwango Sanchez.
Wakati nyota huyo akisonga mbele, ndugu yake na bingwa wa zamani wa US Open, Venus Williams alijikuta akitolewa mashindanoni kwa kukubali kichapo cha 6-2 5-7 7-5 kutoka kwa Angelique Kerber.
Nyota namba mbili kwa ubora duniani, Agnieszka Radwanska alilazimika kufanya kazi ya ziada kutoka nyuma na hatimaye kumshinda Mhispania Carla Suarez Navarro kwa 4-6 6-3 6-0.
Kwa upande wake mkali wa mchezo huo raia wa Serbia, Ana Ivanovic aliibuka kidedea na kutinga raundi ya tatu ya michuano hiyo kwa ushindi wa 6-2 6-2 dhidi ya Msweden Sofia Arvidsson.
Katika raundi ya tatu, Ivanovic anatarajia kupata upinmzani mkali kutoka kwa yoso wa miaka 19 Sloane Stephens, yoso aliyeingia katika 50 bora ya wacheza tenisi wanamama, aliyetinga hatua hiyo kwa kumchapa Tatjana Malek wa Ujerumani kwa 5-7 6-4 6-4.
Licha ya kutupwa nje ya mashindano, bingwa mara tano wa Wimbledon Venus alisema; "Nilijihisi Marekani kwa mara ya kwanza " kutokana na aina ya sapoti aliyooneshwa na kutoka kwa mashabiki wa nyumbani kwenye Uwanja wa Arthur Ashe.
"Hii ni mara ya kwanmza ambayo nimecheza hapa na kuona kundi kubwa la mashabiki likiwa nyuma yangu kama hivi. Nilisubiri uungwaji huu kwa muda mrefu, hatimaye nimeupata ingawa matokeo hayakuwa mazuri," alisema Venus.
"Ilikuwa ya kushangaza sana. Nilijisikia kama niliyeshinda dhahabu. Kiukweli ilimaanisha kitu. Kwa sasa naangalia mbele kuona namna navyoweza kutumia ipasavyo sapoti mara mbili yah ii niktakayopata katika michuano ya mwaka ujao nikiwa bora zaidi."
Wakati Serena akisonga mbele, ndugu yake na bingwa wa zamani wa US Open, Venus Williams alijikuta akitolewa mashindanoni kwa kukubali kichapo cha 6-2 5-7 7-5 kutoka kwa Angelique Kerber
NYOTA anayeshika nafasi ya nne katika viwango vya ubora wa tenisi duniani, Serena Williams hakupata shida kufuzu raundi ya tatu ya micuano ya Wazi ya Marekani ‘US Open’ baada ya kupata ushindi wa moja kwa moja dhidi ya Mhispania Maria Jose Martinez Sanchez.
Bingwa huyo wa michuano ya Wimbledon na Olimpiki, alitumia muda wa saa moja na dakika 22 (1:22) kuibuka kidedea kwa seti mbili kwa bila za 6-2 6-4 dhidi ya nyota asiyekuwa na kiwango Sanchez.
Wakati nyota huyo akisonga mbele, ndugu yake na bingwa wa zamani wa US Open, Venus Williams alijikuta akitolewa mashindanoni kwa kukubali kichapo cha 6-2 5-7 7-5 kutoka kwa Angelique Kerber.
Nyota namba mbili kwa ubora duniani, Agnieszka Radwanska alilazimika kufanya kazi ya ziada kutoka nyuma na hatimaye kumshinda Mhispania Carla Suarez Navarro kwa 4-6 6-3 6-0.
Kwa upande wake mkali wa mchezo huo raia wa Serbia, Ana Ivanovic aliibuka kidedea na kutinga raundi ya tatu ya michuano hiyo kwa ushindi wa 6-2 6-2 dhidi ya Msweden Sofia Arvidsson.
Katika raundi ya tatu, Ivanovic anatarajia kupata upinmzani mkali kutoka kwa yoso wa miaka 19 Sloane Stephens, yoso aliyeingia katika 50 bora ya wacheza tenisi wanamama, aliyetinga hatua hiyo kwa kumchapa Tatjana Malek wa Ujerumani kwa 5-7 6-4 6-4.
Licha ya kutupwa nje ya mashindano, bingwa mara tano wa Wimbledon Venus alisema; "Nilijihisi Marekani kwa mara ya kwanza " kutokana na aina ya sapoti aliyooneshwa na kutoka kwa mashabiki wa nyumbani kwenye Uwanja wa Arthur Ashe.
"Hii ni mara ya kwanmza ambayo nimecheza hapa na kuona kundi kubwa la mashabiki likiwa nyuma yangu kama hivi. Nilisubiri uungwaji huu kwa muda mrefu, hatimaye nimeupata ingawa matokeo hayakuwa mazuri," alisema Venus.
"Ilikuwa ya kushangaza sana. Nilijisikia kama niliyeshinda dhahabu. Kiukweli ilimaanisha kitu. Kwa sasa naangalia mbele kuona namna navyoweza kutumia ipasavyo sapoti mara mbili yah ii niktakayopata katika michuano ya mwaka ujao nikiwa bora zaidi."
August 30, 2012
MTOTO KUWAKILISHA TANZANIA KUPITIA MCHEZO WA ‘TAEKWANDO
Jina: AikaRose Mwasha
Jinsia: Kike
Miaka: 12
Utaifa: TANZANIA
Mchezo: Taekwando
KILO: 28 kg- beginners FEMALE
Club: Nong Jang
Makazi: Leuven Belgium
MAFANIKIO: Medali Ya Fedha & Dhahabu
Kijana wa kitanzania mwenye ndoto ya kuwakilisha nchi yake kwenye mashindano ya kimataifa hapo usoni kwa kupitia mchezo wa mbinu za kujihami wa ‘Taekwando’ ,anamapenzi makubwa na mchezo huu aliouanza angali mdogo akiwa na umri wa miaka 9 ,ameshashiriki mashindano madogo madogo nchini Belgium na kupata mafanikio makubwa kufikia medali ya fedha. Hivi karibuni alifanikiwa kupata medali ya dhahabu katika mashindano ya Olympic open Brussels yaliyofanyika Rue Du Lombartzyde Brussels, Belgium tarehe 27 May 2012.
August 27, 2012
August 21, 2012
August 13, 2012
JAMAICA TAKES GOLD,SILVER & BRONZE IN OLYMPICS 200M
Usain Bolt won the men's 200m in emphatic style tonight, earning his title as the world's greatest ever sprinter. The Jamaican powered home in 19.32 seconds, just a fraction outside the Olympic record of 19.30 - and he raised the roof on the Olympic Stadium by dropping to the track and celebrating by doing press-ups. Yohan Blake and Warren Weir made it a Jamaica one-two-three.
August 9, 2012
OKWI MCHEZAJI BORA WA MWAKA WA SIMBA, APEWA TUZO YAKE ASHANGILIA NA MASHABIKI
Mshambuliaji wa Simba Emmanuel Okwi akionyesha tuzo yake aliyozawadiawa na klabu ya Simba baada ya kuwa mchezaji bora wa mwaka wa klabu hiyo kwenye tamasha la siku ya simba linalofanyika kila mwaka.
Mashabiki nao walinogesha kwa kumuongezea zwadi ya jezi iliyopewa jina la Okwi Hakunaga.




































