May 17, 2013

TASWIRA ZA WASANII WETU WA ZE COMEDI UFUKWENI NI HATARI NA ZINATIA AIBU SANA KWA WANAJAMII

Hi | 3:51:00 PM | | | | | | | | |


 
Katika hali isiyokuwa ya kawaida na kushtua picha zinazowaonesha wasanii wa kundi la Ze Komedi wakiwa kwenye fukwe moja ya huko Kigamboni zimezusha balaa kubwa mtaani huku familia za wasichana hao zilikija juu.

Picha hizo ambazo blog hii ilizinasa kwa gharama kubwa toka kwa mmoja wa wafanyakazi wa fukwe ya Chadibwa zilikopigwa bila kundi hilo kutambua kama walikuwa wanafotolewa picha hizo.


Tangu zimewekwa kwenye blog hii picha hizi zimeanza kusambaa hadi kuwafikia wanafamilia ambao wamekuja juu huku wengine wakitaka kuchukuwa hatua za kuwashtaki wasanii hao kwa udharirishaji wa watoto wao.


Kiongozi wa kundi hilo Mtanga alipotafutwa ili kuzungumzia jambo hili alisema na kueleza kwa ufupi " Kaka hali ya Mungu mimi sijaiona hizo picha hivyo nashindwa kueleza chochote,Isipokuwa kama kuna malalamiko yoyote toka kwa wanafamilia hao wafike ofisini kwetu tuweke sawa" Alisema Mtanga

0 COMMENTS:

Home of Technologies © Copyright 2010-2015 : Designed by : WebMaster