Mlango wa kuingia ndani ya maonyesho Sabasaba
Watu wa rungi nao wapo kwa ajili ya kuhamaisha wadudu warukao na wanaotambaa
DR. Kifimbo kwa ajili ya kila aina ya magonjwa anakukaribisha
Vijana nao wapo kwa ajili ya ulinzi na usalama wa raia wanaoingia na kutoka eneo hilo
Futui nao kutoka kituo cha habari Star TV wapo na wanatumbuiza kwa vichekesho
Siku ya leo nilipa wasaa wa kwenda kunyoosha macho yangu katika maonyesho ya Afrika Mashariki Jijini Mwanza katika Viwanja vya Sabasaba, Watu ni wengi sana na wengi wao wanaonekana walikusudia kuja kufanya mahemezi mbali mbali kwa ajili ya familia zao na biashara kwa ujumla. Hali kwa kweli inalidhisha na amani imetawala, Nilijaribu kupita karibu mabanda 10 yaliyokuja kwa ajili ya maonyesho sehemu hiyo, Na ndipo nilifanikiwa kuchukua baadhi ya matukio kama unavyoona pichani.
Karibu Sabasaba ewe mwananchi ya Mwanza usipitwe na mengi.
0 COMMENTS:
Post a Comment