Hivyo wewe ukiwa kama mwaajili wa mtoto wa ndani mpatie ridhaa mtoto huyo ili ajipatie uzoefu ambao utamsaidia baadaye katika maisha yake, Hatubomoi ila tunawajengea pia uwezo wa kushi vema na waajili wao na kutambua haki zao za msingi wanapokuwa kwa waajili wao, Kushiriki ni bure wala hakuna kiingilio chochote cha pesa au njia yoyote ya malipo kwa mfanyakazi wa ndani, zaidi ni kuzingatia masharti na kuja kwa wakati aliochagua mwenye, Zaidi ni kujaza fomu ambayo itamtambulisha yeye kama mmoja wa washiriki wa watoto wafanyakazi wa ndani katika Shirika hilo, Wanapatikana Isamilo Jijini Mwanza “Tuwape sauti watoto wafanyakazi wa ndani”
Karibuni sana kwa mawasiliano zaidi S.L.P 11348 Namba ya simu +255 717-118087 na +255713-137222 Mwanza-Tanzania.
Hawa ni baadhi ya wanafunzi ambao wanapata mafunzo mpaka sasa ya cherehani.
Mwanafunzi katika mafunzo ya kompyuta akiwa anajifunza mwenyewe baada ya kupata uzoefu toka kwa mwalimu wa mafunzo.
Mwanafunzi akiwa anashona kwa umakini sana na akitabasamu juu ya ujuzi alionao sasa.
Huyu ni mkurugenzi mtendaji wa Shirika hilo linaloitwa Chezesha Mikono akitoa maelekezo kwa mwanafunzi juu ya ushonaji wa nguo.
Mwanafunzi akitengeneza kikapu kwa umahili sana na anafuraha sana
Kijana huyu anajituma sana tena kwa bidii katika mafunzo yake ya kila siku katika shirika hilo.
Mwalimu wa wanafunzi hao akionyesha uwezo alionao katika kushona nguo
Picha na Habari: Ramso Kassim Jijini Mwanza.
1 COMMENTS:
Pongezi kwa kazi nzuri ya kukusanya taarifa.
Post a Comment