June 11, 2013

MSANII WA BONGO MOVIES JAJI KHAMIS KASHI AFARIKI DUNIa KATIKA HOSPTALI YA TAIFA YA MUHIMBILI

Hi | 11:15:00 AM | | | | |
Habari iliyotufikia hivi punde ni kwamba msanii wa filamu nchini Jaji Khamis (Kashi)aliyewahi kutamba na michezo ya ITV enzi zile akiwa na wasanii kama mzee masinde,samson na wengine katika mchezo wa Tamu chungu na mingine mingi Amefariki dunia mchana huu katika hosptali ya taifa ya muhimbili alikokuwa amelazwa.

Taarifa za awali zinasema kuwa alikuwa amelazwa hapo kwa muda kiasi kabla ya kufikwa na mauti hayo. Tutaendelea kuwajulisha zaidi punde tutakapoendelea kupata taarifa zaidi.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Ameni

0 COMMENTS:

Home of Technologies © Copyright 2010-2015 : Designed by : WebMaster