August 3, 2015

ONYO KWA WANAOANGALIA TOVUTI ZA NGONO KWENYE SIMU

Hi | 6:16:00 PM | |
Watafiti toka kampuni ya utafiti ya  Zscalar  wamegundua kuwa,tovuti za kichina zenye picha za ngono zimekuwa zikisambaza virusi ambavyo vinasababisha simu za mikononi kushambuliwa na virusi vya komputa viitwavyo malware.

Utakapotembelea tovuti hizo na ukajaribu kuangalia video,tovuti itakuomba upakue sehemu ya program ya komputa ambayo kiuhalisia ni kirusi kiingine kiitwacho trojan.

Kirusi hicho cha Trojan kinajishajilisha chenyewe kwenye simu yako na kuifanya simu yako kuwa na uwezo wa kupokea matangazo yanayohusisha  ujumbe mfupi wa maneno (sms) ulioko kwenye simu yako.Jambo ambalo litasaidia wahalifu wa mtandao kudukua taarifa zako za kibenki kwenye simu iliyo na kirusi hicho kiurahisi.

0 COMMENTS:

Home of Technologies © Copyright 2010-2015 : Designed by : WebMaster