January 18, 2014

HIKI NI KIZAZI CHA NYOKA KILICHOLAANIWA MSANII KANYE WEST AANZISHA DINI YAKE IITWAYO YEEZIANITY YEYE AJIITA NI MUNGU WA DINI HIYO

Hi | 7:22:00 PM | | |
 Kanye West amepata dini yake iitwayo Yeezianity, “I AM a God,” Kanye West anasikika kwenye moja ya nyimbo zake zilizopo kwenye album Yeezus (jina likiwa mchanganyiko wa aka ‘Ye – na Jesus).
Na sasa wafuasi wa rapper huyo wameanzisha website, Yeezianity.com maalum kwa watu wote wanaotaka kubadilisha dini kwenda Yeezianity, inayojitangaza kama “THE BEST CHURCH OF ALL TIME!
“Sisi ni kundi lisilotaka kujulikana linaloamini kuwa yule anayejiita Yeezus ni kiumbe kitakatifu kilichotumwa na Mungu kuongoza kwenye kizazi kipya cha ubinadamu,” yanasomeka maneno kwenye website.

Kwenye website hiyo kuna sheria kadhaa au nguzo na tamko la imani likiwemo ‘Imani kwa Yeezus’ na ‘I believe Yeezus will lead us into a new Age of Creativity’. Amen.” Mwanzilishi wa ‘Yeezianity’ ameongea na mtandao wa Vice kwa masharti ya kutotajwa jina na kusema kuwa Yeezianity si kitu cha mzaha
 Ukitaka kujiunga na dini hiini rahisi sana.Unachotakiwa kufanya ni kuwatumia email yenye picha isiyokutambulisha ukiwa umeshika karatasi lililoandikwa ‘I Believe In Yeezus’.

0 COMMENTS:

Home of Technologies © Copyright 2010-2015 : Designed by : WebMaster