January 13, 2013

VENGU WA ORIJINO KOMEDY KWA SASA ANAENDELEA VYEMA

Hi | 12:13:00 AM | | |
Baada ya minongono mingi kuhusiana na hali ya msanii mwenzao Vengu, hatimaye memba wa kundi ya Ze Orijino Komedy Masanja mkandamizaji amefunguka na kueleza kuwa msanii mwenzao Joseph Shamba aka Vengu anaendelea vizuri baada ya kurejea kutoka India alikokuwa akitibiwa.
akiandika kwenye ukurasa wake wa Facebook leo Masanja amesema kuwa Vengu bado anaendelea kupata matibabu akiwa nyumbani “Ukweli ni kwamba Ndugu yetu Joseph Shamba (Vengu) yuko nyumbani akiendelea na matibabu yake na uangalizi wa mara kwa mara kwa madaktari baada ya kurejea kutoka India.” alisema masanja na kuongeza “…Muda mwingi tuko naye na tunazidi kumuombea apone na arejee kutoa burudani. Na mnaomuombea mabaya na kumzushia habari za kila aina tunawakabidhi kwa Mungu awajalie busara.”
Habari hizi zimekuja wakati mzuri kwani habari za kuugua na ugonjwa wa Vengu upatikanaji wake si wa wazi licha ya mashabiki na jamii kufahamu kuwa Vengu anaumwa basi.
Tunamuombea mwenyezi Mungu amjalie mja wake aweze kupona na kurejea kazini kulitumikia taifa na jamii kwa ujumla.

0 COMMENTS:

Home of Technologies © Copyright 2010-2015 : Designed by : WebMaster