December 8, 2012

TASWIRA ZA FM ACADEMIA WAPAGAWISHA NA VUNDES MOSHI

Hi | 3:11:00 PM | | | | | | |
Wakiongozwa na Rais wa Bendi hiyo kongwe katika tasnia ya Muziki wa Dansi hapa nchini Nyosh El Sadaat, vijana hao maarufu kama wazee wa Pamba, walishambulia jukwa la ukumbi huo majira ya nne usiku kwa kuporomosha baadhi ya nyimbo zao za zamani na nyimbo mbili kutoka katika album mpya ya Chuki ya Nini.
Badhi ya nyimbo zilizopigwa katika shoo hiyo ni pamoja na Vuta ni kuvute, iliyo kwenye album ya Vuta nikute, Anna, Maisha Kigeugeu kabla ya kuuteka ukumbi huo uliofurika wapenzi wa muziki wa Dansi kutoka Moshi na Arusha kwa kucheza Staili yao mpya ya Vundes na nyimbo mpya mbili, Maisha uliotungwa na Pablo Maasai na wimbo wa Ndoa ya Kisasa uliotungwa na Mulemule.
“Vundes ni Ubunifu na moja ya vitu vikali tuliomua kuwaletea nah ii ni kuhakikisha wazee wa Ngwasuma, tunayendelea kuwateka na kuwa nambari wani kwenye muwa dansi, Vundes inamaanisha makalio, ndio maana tunaimba akina dada wanapenda kucheza vundes na akina kaka wanapenda kuangalia vundes, alisema Nyoshi

0 COMMENTS:

Home of Technologies © Copyright 2010-2015 : Designed by : WebMaster